NUSU YA SIMBA WOTE DUNIANI WAKO TANZANIA.

RAIS wa Jumuiya ya Uwindaji ya Kimataifa, (SCI), Sven Lindqueast ameitaja Tanzania kuwa ni nchi yenye  nusu ya simba wote Duniani katika Mkutano wa 50 wa Mwaka wa Uwindaji wa Kitalii unaoendelea kufanyika nchini hapa. Rais huyo Bw. Sven Lindquest amesema kwa hatua hiyo ameipongeza kwa juhudi za utunzaji na kupelekea wingi wa wanyama hao.